Obama na Michelle Obama watoa wito kwa Wamarekani kuunga mkono ‘ukurasa mpya‘ na Harris

 

Obama na Michelle Obama watoa wito kwa Wamarekani kuunga mkono ‘ukurasa mpya‘ na Harris

g

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Obama amewaahidi Wanademocrat kwamba Harris "atazingatia matatizo yako" na "hatashughulikia tu wapiga kura wake na kuwaadhibu wale wanaokataa kupiga goti."

Wawili hao walikuwa wakizungumza kwenye kongamano la Democrat ambapo wamemuunga mkono Kamala Harris kama mgombea wa urais wa chama hicho.

Obama pia anasema anampenda Tim Walz, ambaye amesema ni "aina ya mtu anayepaswa kuwa katika siasa - mtu ambaye alizaliwa katika mji mdogo, aliitumikia nchi yake, alifundisha watoto, alifundisha soka, na kuwajali majirani zake."

"Anajua yeye ni nani na ni nini muhimu."

Obama aliendelea kusema kuwa kuwachagua Harris na Walz "haitakuwa rahisi".

"Kazi yetu ni kuwashawishi watu kwamba demokrasia inaweza kuleta mafanikio," amesema.

"Kamala anaelewa hili," anasema.

Wakati huo huo Michelle Obama amesema kwamba Harris ni "mmoja wa watu wenye uwezo kuwahi kugombea wadhifa wa urais".

"Na yeye ni mmoja wa watu wenye hadhi kubwa, heshima kwa mama yake, kwa mama yangu, na pengine kwa mama yako pia," Obama anaongeza. "Mfano wa hadithi tunazojieleza kuhusu nchi hii."

Obama anasema kwamba "hadithi yake ni hadithi yako. Ni hadithi yangu. Ni hadithi ambazo Wamarekani wengi wanaojaribu kujenga maisha bora".

Comments

Popular posts from this blog

Hukumu aliyopewa mwanamume aliyembaka na kumuua muathiriwa yazua ghadhabu Ethiopia

Marekani inarudia makosa ya USSR katika Mashariki ya Kati

Putin anaweka wazi kuwa mazungumzo na Kiev sasa hayawezekani - Lavrov